MAFUNZO
Mafunzo yatolewayo na baraza yanalenga kuboresha uwezo na utendaji wa watendaji katika Sekta ya Ujenzi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Mafunzo hayo husaidia katika upatikanaji wa mbinu bora zinazohitajika katika uboreshaji wa huduma, hivyo kuimarisha ushindani na kuhakikisha thamani ya pesa kwenye miradi inayojengwa.
Baraza linaendelea kutekeleza mipango kadhaa ya mafunzo kwa vitendo. Maeneo mahususi yanayozingatiwa ni pamoja na: Manunuzi ya Umma, Usimamizi wa Mikataba na Miradi ya Ujenzi, Makadirio ya Gharama za Ujenzi, Kaguzi za Kiufundi, Usuluhishi wa Migogoro katika utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (Usuluhisi nje ya Mahakama), Madai katika Miradi ya Ujenzi, Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Teknolojia ya nguvu kazi katika ukarabati wa Barabara, Ukarabati wa Majengo.
Baraza pia huendesha mafunzo kulingana na huitaji wa wateja.
Mafunzo yatolewayo na Baraza hulenga washiriki kutoka fani mbalimbali zikiwemo: Wahandisi, Wasanifu Majengo, Wakadiriaji Majenzi, Wathamini, Wasimamizi wa Majengo, Wataalamu wa Bima, Wahasibu, Wanasheria, Wakadiriaji Vipimo, Maafisa Ununuzi na Ugavi, Maafisa Mipango, Washauri Elekezi na Mafundi.
MAFUNZO TUNAYOTOA
MIKATABA YA JENGA SANIFU
Malengo ya mafunzo
Mafunzo haya yanawapa washiriki ujuzi juu ya kanuni za kusanifu na Kujenga; manunuzi ya huduma za Sanifu Jenga, mikataba ya huduma ya Sanifu Jenga, Utekelezaji na ukamilishaji wa Miradi ya Sanifu-Jenga Usuluhishi wa migogoro, Changamoto zinazoonekana kwa miradi inayotekelezwa chini ya usanifu na ujenzi na kuhakikisha kuwa changamoto zinamalizika au kupunguzwa kwa kiasi kikubwa.
Mada:
MUDA: Siku 5
NJIA ZA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA GHARAMA KATIKA MIKATABA YA UJENZI
Lengo la Mafunzo
Mafunzo haya yatawapa washiriki ujuzi wa kukabiliana na mabadiliko ya gharama katika mikataba ya ujenzi.
Mada:
MUDA: Siku 5
USULUHISHI WA MIGOGORO KATIKA MIKATABA YA UJENZI
Malengo ya mafunzo:
Mafunzo haya yatawapa washiriki ujuzi na maarifa kwa njia ya vitendo juu ya utatuzi wa migogoro katika mika-taba ya ujenzi kwa njia ya usuluhishi na njia nyingine mbadala (ADR).
Mada
MUDA: Siku 3
USIMAMIZI WA MABADILIKO YA KAZI, MADAI NA MIGOGORO
Malengo ya mafunzo:
Mafunzo haya yatawapa washiriki ujuzi unaohitajika katika kusimamia mabadiliko ya kazi jinsi ya kusimamia madai na migogoro katika miradi ya ujenzi.
Mada:
MUDA: Siku 5
USIMAMIZI WA MKATABA YA UJENZI
Madhumuni ya Mafunzo:
Mafunzo haya yatawapa washiriki ujuzi wa usimamizi bora wa mikataba ya ujenzi.
Mada:
MUDA: Siku 5
MAKADIRIO YA KAZI ZA UJENZI WA BARABARA
MUDA: siku 5
Fahirisi za Gharama za Ujenzi Tangu 1990 Baraza limekuwa likizalisha fahirisi...
Usuluhishi wa Migogoro Tangu mwaka 1982 Baraza limekuwa likiratibu migogoro k...
Utafiti Kazi za utafiti zinazolenga katika kutambua matatizo mbalimbali na uf...