Tunu za Taasisi
Katika kutekeleza dira, dhima na majukumu yake, Baraza linaongozwa na tunu zifuatazo:
- Huduma Bora
- Uadilifu
- Ushirikiano
- Ubunifu
- Weledi
- Uwazi
- Uwajibikaji
Kanuni
- Kutambua na kukubali wajibu wetu kwa taifa wa kuhakikisha kuwa miradi ya miundombinu ya kijamii na kiuchumi inaendelezwa na kudumishwa kwa ufanisi ili kutimiza malengo yaliyokusudiwa.
- Kutoa miongozo, uwajibikaji na uwezo kwa tasnia, katika kuhakikisha ufanisi na uchumi vinapatikana.
- Kutoa huduma bora kwa wateja kwa ufanisi.
- Kujiendeleza kiteknolojia katika kutoa huduma bora.
- Kuongeza ujuzi na uzoefu kwa wafanyakazi wetu kupitia mafunzo mbalimbali
- Kuwapatia wadau wa sekta ya ujenzi fursa sawa katika kutekeleza majukumu yao.