Utangulizi

Mafunzo ni muhimu sana katika kukuza uwezo wa wadau wa sekta ya ujenzi. Mafunzo yanasaidia utendaji bora wa kazi ambao ni muhimu katika kukuza na kuongeza ubora na tija, pia kuwezesha kukabiliana na ushindani na kuleta thamani halisi kwa fedha zilizotumika katika miradi ya ujenzi.

Baraza linaendesha mafunzo kwa njia ya vitendo katika nyanja mbalimbali zinazohusiana na ujenzi zikijumuisha: ununuzi, usimamizi wa mikataba, usimamizi wa miradi, ukadiriaji wa gharama za ujenzi, sheria zinazohusiana na mikataba ya ujenzi,ukaguzi wa kiufundi, usuluhishi wa migogoro, menejimenti ya madai, mafunzo kwa makandarasi, ubia kati ya sekta binafsi na ya umma, ujenzi na matengenezo ya barabara kwa kutumia teknolojia ya nguvu kazi, matengenezo ya majengo pamoja na matumizi ya kompyuta katika ukadiriaji wa bei za majenzi na usimamizi wa miradi ya ujenzi.

Mafunzo pia yanatolewa kwa watu wenye mahitaji maalum kufuatana na mahitaji yatakayowasilishwa (Tailor made courses).